• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

Ifahamu programu ya BOOST

Posted on: December 16th, 2022

Malengo ya uanzishwaji wa Programu(MUP)

Malengo ya programu ni kuwezesha upatikanaji wa fursa sawa katika ujifunzaji bora wa Elimu ya awali na msingi Tanzania Bara. BOOST ni sehemu ya mpango wa Lipa kutokana na matokeo katika Elimu awamu ya pili(EPforR II) na inachangia katika utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa sekta ya elimu wa miaka mitano 2021/22 hadi 2025/26


Matokeo muhimu

Vyumba vipya vya madarasa 12,000 kujengwa na vifaa vya shule vinavyohusika katika maeneo yenye uhitaji zaidi


Vituo 800 katika shule za msingi /vituo vya walimu kuanzishwa na kuendelezwa kwa ajili ya utoaji wa mafunzo kwa njia ya TEHAMA kupitia maktaba mtandao/kielektroniki na mfumo wa usimamizi wa ujifunzaji kimtandao


Shule za msingi 6,000 kuwezeshwa kutekeleza programu ya shule ya msingi salama.


Madarasa 12,000 ya elimu ya awali yaliyoboreshwa pamoja na njia bora za ufundishaji vikiwemo vifaa vya ujifunzaji


Kuongezeka kwa uwiano wa uandikishaji wa wanafunzi wa elimu ya awali kutoka asilimia 76.9 hadi asilimia 85.


Kuongezeka kwa uwiano wa uandikishaji wa wanafunzi wa elimu ya awali kutoka asilimia 57.5 hadi asilimia 65.6 kwa Halmashauri zilizo katika kundi la robo ya chini


Kuongezeka kwa kiwango cha wanafunzi kubaki shuleni kwa Halmashauri zilizo katika kundi la robo ya chini kutoka asilimia 55.9 hadi asilimia 66.24


Asilimia 50 ya wanafunzi wa darasa la pili kufikia kiwango cha chini cha kumudu stadi za kusoma na kuandika na asilimia 35 katika kuhesabu


Ushiriki wa walimu katika mpango wa mafunzo Endelevu ya walimu kazini (MEWAKA) kufikia asilimia 50


Kuimarisha mfumo katika:

Takwimu, mipango, ufuatiliaji na tathimini ya maendeleo ya sera yanayotokana na ushahidi


Maendeleo ya sera yanayotokana na uthibitisho


Ujenzi wa miundombinu kwa kushirikisha jamii


Uwezo wa kitaifa katika uandaaji wa mitaala na upimaji katika ujifunzaji


Umahiri wa matumizi ya TEHAMA kwa wanafunzi na walimu wa shule za msingi


Mfumo wa kitaifa wa mafunzo endelevu ya walimu kazini(MEWAKA)


Kuimarisha maktaba mtandao na mfumo wa usimamizi katika ujifunzaji


Halmashauri zinazozingatia utawala bora katika elimu


Maendeleo ya elimu yanayozingatia mazingira na hali za jamii


Hii ndio programu ya BOOST, ambayo hivi leo Afisa Elimu Mkoa wa Tanga Mwalimu Newaho Mkisi amefungua mafunzo ya siku mbili kwa watumishi 234 wa kada teule kutoka Halmashauri 18 za mikoa ya Kilimanjaro na Tanga, watumishi wa ofisi za wadhibiti ubora elimu, watumishi wa ofisi za TSC na wale wa sekretarieti za mikoa, yatakayofanyika katika Ukumbi wa Shule ya wasichana Korogwe mkoani Tanga, yakiwa na shabaha ya kuwajengea uwelewa wa programu ya BOOST na uwezo kabambe wa kwenda kutekeleza malengo ya programu hiyo.

Mratibu msaidizi wa programu ya BOOST kitaifa kutoka Ofisi ya Rais-TAMISEMI  Ndugu. Reuben Swilla akizungumza mbele ya mgeni rasmi katika ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo watumishi kuhusu program ya BOOST.


Afisa Elimu Mkoa wa Tanga na Mgeni rasmi Mwalimu Newaho Mkisi katika ufunguzi wa mafunzo ya program ya BOOST kwa watumishi wa Halmashauri na Sekretarieti za mikoa ya Tanga na Kilimanjaro akizungumza na washiriki.


Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo, mgeni rasmi na Afisa Elimu mkoa wa Tanga amewasihi sana washiriki wa mafunzo hayo, kuzingatia weledi, ushirikiano wa hali ya juu miongoni mwao watakaporudi kutekeleza malengo ya programu katika maeneo yao.

Washiriki wa mafunzo ya programu ya BOOST wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo ya siku mbili


Mwandishi wetu

Handeni mji

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI UJENZI WA JENGO LA DHARURA (EMD) HOSPITALI YA WILAYA HANDENI February 16, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • Afisa elimu msingi: Kula shuleni ni lazima

    March 13, 2023
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yafana, Halmashauri ya Mji Handeni

    March 08, 2023
  • Walimu Halmashauri ya Mji Handeni, wapata mafunzo ya mfumo wa FFARS

    March 04, 2023
  • MILIONI 63.6 ZAMWAGWA KWA WAJASIRIAMALI HANDENI MJI. RAIS SAMIA ATAJWA.

    March 03, 2023
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.